Kanuni za Ligi na Usajili 2023/24

TAVA yaendelea kuboresha sheria na kanuni zinazoongoza mpira wa wavu nchini - ikigusia msimu wa mashindano, mfumo, mahitaji na ada za usajili kwa mwaka 2023.

1 min

Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania, TAVA, kimefanya maboresho ya Kanuni za Usajili za Mwaka 2022 Toleo la Mwezi Februari ili kukidhi mahitaji ya wakati. Kwa kuzingatia kanuni hizi, TAVA inalenga kusimamia haki na wajibu wa kila mshiriki huku ikilinda hadhi zao nyakati zote. Utekelezaji na usimamizi wa Sheria, Kanuni na Miongozo utaanzia ngazi ya Timu/ Klabu, Wilaya, Mkoa, Kamisheni husika ambapo ngazi ya Mwisho niofisi ya Sekretarieti ya TAVA.

Pakua nakala ya Kanuni za Ligi na Usajili 2023/24 hapa.

More News

Blog details image
News and Updates
Arrow Icon

TVF Calendar Activities 2026

Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania (TVF) limetangaza kalenda yake kamili ya shughuli za mwaka 2026, ikiwa na zaidi ya mashindano 25 ya kitaifa na kimataifa. Kalenda hiyo inajumuisha Ligi ya Taifa (TVNL), Kombe la Taifa, Bingwa wa Afrika kwa wanawake na wanaume, mashindano ya vijana, na shughuli nyingine zinazoendelea katika miji mbalimbali ikiwemo Dar es Salaam, Dodoma, Mwanza, na Zanzibar. Pakua kalenda ili usikose tukio lolote la mpira wa wavu mwaka huu.

Blog details image
Uchaguzi
Arrow Icon

Matokeo ya Mchujo wa Wagombea: Magoti Apitishwa Kugombea Urais, Joseph John Akosa Sifa

TVF imetoa matokeo ya uchunguzi wa sifa za wagombea wa uongozi ambapo baadhi wamepitishwa na wengine wamekatwa. Kamati imetoa utaratibu wa pingamizi na rufaa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi.

Blog details image
Uchaguzi
Arrow Icon

Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania (TVF) Kufanyika Desemba 21, 2025 Jijini Dodoma

TVF imetangaza uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 21 Desemba 2025 jijini Dodoma. Fomu zinapatikana kuanzia tarehe 10 Novemba hadi 24 Novemba 2025 kupitia tovuti ya TVF. Wadau wote wa mpira wa wavu wanahimizwa kushiriki kwa kuchukua na kurejesha fomu kwa wakati.