TAVA yaendelea kuboresha sheria na kanuni zinazoongoza mpira wa wavu nchini - ikigusia msimu wa mashindano, mfumo, mahitaji na ada za usajili kwa mwaka 2023.
1 min
Chama cha Mpira wa Wavu Tanzania, TAVA, kimefanya maboresho ya Kanuni za Usajili za Mwaka 2022 Toleo la Mwezi Februari ili kukidhi mahitaji ya wakati. Kwa kuzingatia kanuni hizi, TAVA inalenga kusimamia haki na wajibu wa kila mshiriki huku ikilinda hadhi zao nyakati zote. Utekelezaji na usimamizi wa Sheria, Kanuni na Miongozo utaanzia ngazi ya Timu/ Klabu, Wilaya, Mkoa, Kamisheni husika ambapo ngazi ya Mwisho niofisi ya Sekretarieti ya TAVA.
Pakua nakala ya Kanuni za Ligi na Usajili 2023/24 hapa.
TVF imetoa matokeo ya uchunguzi wa sifa za wagombea wa uongozi ambapo baadhi wamepitishwa na wengine wamekatwa. Kamati imetoa utaratibu wa pingamizi na rufaa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi.
TVF imetangaza uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 21 Desemba 2025 jijini Dodoma. Fomu zinapatikana kuanzia tarehe 10 Novemba hadi 24 Novemba 2025 kupitia tovuti ya TVF. Wadau wote wa mpira wa wavu wanahimizwa kushiriki kwa kuchukua na kurejesha fomu kwa wakati.
Hati mpya kupatikana kwenye tovuti zikiwemo: Kanuni za Ligi na Usajili [2025], Kanuni za Maadili, Kanuni za Uchaguzi, Kanuni za Fedha na Utawala (Machi 2025) na Katiba ya hivi karibuni [Toleo la 2023]