Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania (TVF) imetangaza rasmi majina ya wagombea waliopitishwa na waliokosa sifa za kugombea uongozi katika uchaguzi mkuu ujao. Soma hapa kuona orodha kamili, sababu za kisheria, na utaratibu wa kuwasilisha pingamizi au rufaa.
3 min
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania (TVF), chini ya Mwenyekiti wake Pius Joseph, imetoa matokeo ya utahini wa wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi wa shirikisho hilo.
Mchakato huo umefanyika kwa kuzingatia Kanuni ya 11 (1) na (2) ya Kanuni za Uchaguzi wa TVF. Katika matokeo hayo, baadhi ya wagombea wamepitishwa huku mmoja akitajwa kukosa sifa za kuendelea na kinyang'anyiro hicho.
Hapa chini ni mchanganuo wa maamuzi ya kamati kwa kila nafasi:
1. Nafasi ya Rais
- Magoti Hongora Mtani: Amepitishwa
- Joseph K.E. John: Amekosa sifa, kulingana na kanuni ya 10.3 na 10.4
2. Nafasi ya Makamu wa Rais
- Saumu Agapa: Amepitishwa
3. Wajumbe wa Bodi (Wanawake)
- Julieth Julius Tibanywana: Amepitishwa.
- Mwajuma Issa: Amepitishwa.
4. Wajumbe wa Bodi (Wanaume)
- Auxillius M. Audax: Amepitishwa.
- Julius Kisagero: Amepitishwa.
Kamati ya Uchaguzi imetangaza ratiba na utaratibu maalum kwa ajili ya wagombea na wadau wasioridhika na matokeo haya:
A. Pingamizi (Kwa waliopitishwa)
Kamati inatoa haki ya kuweka pingamizi dhidi ya wagombea waliopitishwa.
Tarehe: Kuanzia 30/11/2025 hadi 01/12/2025.
Muda wa Mwisho: Saa 10:00 Jioni.
Jinsi ya Kuwasilisha: Pingamizi lazima liwe la maandishi na kutumwa kupitia barua pepe: uchaguzi@tvf.or.tz.
B. Rufaa (Kwa wasiopitishwa)
Wagombea wasiopitishwa wana haki ya kukata rufaa kwa kuzingatia Kifungu cha 12 cha Kanuni za Uchaguzi.
Tarehe: Kuanzia 07/12/2025 hadi 09/12/2025.
Muda wa Mwisho: Saa 10:00 Jioni.
Jinsi ya Kuwasilisha: Rufaa lazima ziwe za maandishi na kutumwa kupitia barua pepe: uchaguzi@tvf.or.tz
TVF imetangaza uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 21 Desemba 2025 jijini Dodoma. Fomu zinapatikana kuanzia tarehe 10 Novemba hadi 24 Novemba 2025 kupitia tovuti ya TVF. Wadau wote wa mpira wa wavu wanahimizwa kushiriki kwa kuchukua na kurejesha fomu kwa wakati.
Hati mpya kupatikana kwenye tovuti zikiwemo: Kanuni za Ligi na Usajili [2025], Kanuni za Maadili, Kanuni za Uchaguzi, Kanuni za Fedha na Utawala (Machi 2025) na Katiba ya hivi karibuni [Toleo la 2023]
Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania – TVF, linawataarifu wadau wote kuwa dirisha la usajili kwa Vituo na Shule za kulelea Watoto, Taasisi binafsi, Makocha na Waamuzi limefunguliwa kuanzia leo tarehe 2/2/2024 hadi tarehe 16/2/2024.