Kufunguliwa Kwa Dirisha La Usajili Kwa Vituo Na Shule Za Kulelea Watoto, Taasisi Binafsi, Makocha Na Waamuzi

Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania – TVF, linawataarifu wadau wote kuwa dirisha la usajili kwa Vituo na Shule za kulelea Watoto, Taasisi binafsi, Makocha na Waamuzi limefunguliwa kuanzia leo tarehe 2/2/2024 hadi tarehe 16/2/2024.

3 min

Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania – TVF, linawataarifu wadau wote kuwa dirisha la usajilikwa Vituo na Shule za kulelea Watoto, Taasisi binafsi, Makocha na Waamuzilimefunguliwa kuanzia leo tarehe 2/2/2024 hadi tarehe 16/2/2024.

Hivyo basi, kwa wale ambao walikuwa hawajasajili bado taasisi zao na ambao walikuwa hawajakamilisha taratibu za kusajili watumie dirisha hili kukamilisha zoezo hilo.

Makochana Waamuzi: baadhi ya makocha na waamuzi wamefanikiwa kusajiliwa kikamilifu na wengine walikutana na changamoto mbalimbali katika kusajili wanatakiwa kuingia kwenye mfumo kwa ajili ya kurekebisha taarifa zao na kuna wengine ambao walilipia na hawakufanikiwa kukamilisha usajili nao wanatakiwa kuingia kwenye mfumo kwa ajili ya kukamilisha usajili wao pia ambao hawajasajili kabisa wanatakiwa wajisajili mapema kabla ya muda wa dirisha kufungwa.

Wahusikawote mnasisitizwa kujisajili mapema kwa ajili ya kupata vibali vya kushirikishughuli zote zinazosimamiwa na Shirikisho la Mpira wa Wavu – TVF

Link za usajili

👉🏽 Taasisi binafsi

👉🏽 Shule na Vituo vya Kukuza Vipaji

👉🏽 Makocha

👉🏽 Waamuzi

Kwa changamoto zozote za kimfumo na kiufundi wasiliana na namba zifuatazo

+255 764 600 741 – Mkurugenzi wa Ufundi

+255 764 837 005 – Afisa TEHAMA (IT)

Imetolewa na Idara ya Habari na Mawasiliano

More News

Blog details image
Uchaguzi
Arrow Icon

Matokeo ya Mchujo wa Wagombea: Magoti Apitishwa Kugombea Urais, Joseph John Akosa Sifa

TVF imetoa matokeo ya uchunguzi wa sifa za wagombea wa uongozi ambapo baadhi wamepitishwa na wengine wamekatwa. Kamati imetoa utaratibu wa pingamizi na rufaa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi.

Blog details image
Uchaguzi
Arrow Icon

Uchaguzi Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Wavu Tanzania (TVF) Kufanyika Desemba 21, 2025 Jijini Dodoma

TVF imetangaza uchaguzi mkuu utakaofanyika tarehe 21 Desemba 2025 jijini Dodoma. Fomu zinapatikana kuanzia tarehe 10 Novemba hadi 24 Novemba 2025 kupitia tovuti ya TVF. Wadau wote wa mpira wa wavu wanahimizwa kushiriki kwa kuchukua na kurejesha fomu kwa wakati.

Blog details image
News and Updates
Arrow Icon

Hati Muhimu Mpya Kwajili ya Msimu 2025

Hati mpya kupatikana kwenye tovuti zikiwemo: Kanuni za Ligi na Usajili [2025], Kanuni za Maadili, Kanuni za Uchaguzi, Kanuni za Fedha na Utawala (Machi 2025) na Katiba ya hivi karibuni [Toleo la 2023]